JINSI YA KUITA JINI KUTOKA KABURINI


Watu wengi wanadhani majini wanaishi baharini pekee, laah majini wanaishi popote na wanauwezo wa kuishi popote ambapo anaishi kiumbe yoyote sababu wao wanauwezo wa kugeuza maumbile yao katika kila aina ya mnyama, mdudu au mimea.

Karibu darasani leo na Maalim amekuandalia somo pevu lenye maarifa jinsi ya kumuita na kumtumia jini kutoka kaburini. Usisahau kusubscribe kukoment na kushare maarifa haya ili na wenzetu wengine yawafikie pia ukivutiwa sana na darasa hili muandikie ujumbe Maalim Shafii Neyz katika nambari +255 692 007 575

Maalim Shafii somo la leo ameliandaa kwa njia ya simulizi, ni masuala mtambuka yanahitaji umakini mkubwa sana. Siku moja Maalim Shafii The Don alikuwa katika shughuli zake za kuandaa dawa ambapo watu wake wa kichwa walimuelekeza kuwa dawa hiyo itapatikana katika kabuli la shujaa wa nchi fulani ambapo kabuli hilo mtu wa kawaida akifika kutazama huwa halionekani.

Kwa sababu maalum Maalim Shafii hakusema kabuli hilo lipo nchi gani, aliendelea kusimulia ya kuwa ukifika nchi hiyo wazawa husema kabuli ya mmoja wa mababu zetu ni tiba ila kuliona hadi uwe na bahati sana. Maalim alilezwa kabuli lilipo na kuanza safari, ni umbali wa kilomita kama 25 kutoka katika makazi ya watu.

Ukiwa unaelekea katika kabuli hilo kwanza hutakiwi kuwa na najisi mwilini au uwe na nyama mbichi au kiberiti na kisu, vitu hivyo unatakiwa kuviacha sehemu ukapovua viatu. Ni sehemu ya kuogofya sana japo ni sehemu nzuri ingawa haiwezekani kutumika kwa masuala ya kitalii au anasa. Ni bustani hivi na likifika jua la utosi kuna maua yananukia manukato mazuri sana.

Alipofika eneo la kaburi hakuna chochote zaidi ya mti mrefu usio na matunda, alisikia sauti ikimuarisha kutoa heshima. Alipokiri kutoa heshima ghafla akaliona kaburi na kiumbe aliyekuwa akidhaniwa kuwa ni mtu japo miguu yake ilikuwa haionekani vyema.

Ilisikika sauti ikisema;- “Umetoka mbali sana kumtafutia suluhu binti mgonjwa kutoka katika ardhi yako, hili kabuli mimi ndiye mlinzi, kama ungekuwa huna nia njema usingeliona kaburi hili. Hadi kufikia hii leo ni watu watano tu wamefanikiwa kuona hili kabuli tokea huyu kiumbe azikwe hapa.”

Maalim aliogopa sana na kusikiliza maelekezo vyema, alipewa kitu kama majani na karatasi liliondikwa kwa hadi ya kiebrani. Hakuwa na uelewa na lugha ya kiebrani. Ghafla alipigwa na usingizi mzito ambapo anadhani ya kuwa alilala siku nzima bila kushtuka, aliposhtuka alibaini yupo eneo ambalo halina kaburi lakini mkononi ameshikiria kijikaratasi mkononi chenye hati ya kiebrania ambacho mara baada ya kukutana na wakalimani walimsomea na kumueleza kuwa alielekezwa jinsi ya kumuita jini kutoka kaburini.

Ili kumuita jini aliyekabirini ni kama ifuatavyo;-

• Unahitaji mishumaa yenye rangi nyeusi iwe 10 kwa idadi.

• Uchafu wa kaburi yaani taka za kaburi lolote.

• Kikombe cha bati kimoja.

• Chora umbo la Pentagoni lenye ukubwa wa kukaa mtu.

• Weka kikombe na ule uchafu ndani ya Pentagoni.

• Imbilizia maneno maneno haya;- Kiumbe wa kifo, onyesha kisa cha nafsi yangu, hebu fanya maagizo yangu.

Baada ya kuita na ukapata hisia kuna kiumbe amekuja utachukua huo uchafu wa makaburini au michanga uitupe ndani ya Pentagoni kisha utasema maneno haya;-

“Ninao ufunguo, nina nguvu, nifungulie mlango wa kuzimu….”

Milango itafunguka saa saba na utaona joka kubwa likitoka kisha utasema.

“Wewe ni rafiki yangu na mtu wangu, tutiahsi pamoja na utafnya kile ninachokuelekeza, tutaishi pamoja kama marafiki n ahata nikifa utakuwa chini ya watoto wangu.”

Maneno haya utayatamka ukiwa katikati ya mishumaa kwenye umbo la Pentagoni ulilolichora, baada ya kuita ukataa muda kidogo na kuita tena na kama hajaja utatakiwa kuwa na subira na usitoke mpaka aje. Akija hakikisha hakuna mtu mwgingine zaidi yako maana akifika yeye huamini mtu wa mwanzo kumuona ndiye mfamle wake na anatakiwa kutii amri zake. Unaweza kupoteza muda kumuita ila ajaka na akawa hakutii wewe kwani anakuwa amemuona mtu mwingine kabla ya kuona uso wako.

Hivyo ndivyo tafsiri ya yale maneno ya kiebrania yalivyoandikwa, kutoka hapo Maalim Shafii akawa na uwezo wa kuwaita majini waishi makaburini na majini waishi makaburini hawana maelewano mazuri na majini waishio baharini.

Hiyo ilikuwa ni njia ya kuita japo maneno yale ya kiebrani yalienza pia jinsi ya kuondosha ambapo ni kama ifuatavyo;-

• Utaimbilizia maneno haya “Kuanzia sasa utatii amri zangu, nakufungulia mlango utoke na ufike salama tutaonana tena nikikuhitaji”.

• Utamuelekeza aende porini kwenye mapango ambako huko pia umeweka dhahabu. Kwanini unamuwekea dhahabu ni ili kumfanya atulie na ili iwe rahisi kumuita siku nyingine.

Matajiri wengi pesa zao na dhahabu zipo porini wajua kwanini wanazihifadhi huko? Hakikisha jini huyu wa kaburi haumtumii kwa masuala yenye mihemko na hisia, akikisha haumtumii kwa kisasi, au kwa kumtumia kwa ajili ya ngono na hata kama akiwa ni wa jinsi ya kike mwenye uzuri wa kuvutia hakikisha haumuingilii kimwili.

Asante kwa kuwa name na usikose darasa zijazo za Maalim Shafii kwani yeye ni kisima cha maarifa.

Comments

  1. Kweli kumbe binadamu ni kiumbe chenye spiritual power ya kutosha Sana sema wengi hatuzijui Na hatutumii enyi wachache mliotambua Ayo Mungu awape maisha marefu mtufunze Sisi Na vizazi vijavyo umasikini sio mzuri ndugu zangu

    ReplyDelete
  2. Natamani sana kupata elimu hii vizuri kiongoz naomba nipate darasa hili vizuri na elimu ya mamiwata pia

    ReplyDelete
  3. Unamuita muda gani Usiku au mchana na ukiwa wapi ndani au porini

    ReplyDelete
  4. Nadhani tunahitaji elimu zaidi

    ReplyDelete
  5. This comment has been removed by the author.

    ReplyDelete
  6. Ni mambo mazuri sana shida ni uwoga ila ukizoea utaona kawaida elewa 2 kuwa hakuna utajiri kirahisi ndio maana watu wote duniani Wanaitafuta pesa ila hawana njia za elimu hizi ila wengine uwoga pia na maamuzi katika kuyakabiri mafanikio

    ReplyDelete

Post a Comment